Tuesday, 13 May 2014

UN yalaaani shambulizi Somalia

Posted by mkachu  |  Tagged as:


Mji wa Baidoa ulikombolewa na serikali kutoka kwa Al Shabaab miaka 2 iliyopita

Umoja wa Mataifa umelaani shambulizi baya sana la kujitoa mhanga lililotokea eneo la Kati mwa Somalia Jumatatu.
Taarifa kutoka kwa Muungano wa Afrika imesema kuwa watu 19 walifariki katika shambulizi hilo lililotokea mjini
Baidoa mnamo Jumatatu.

Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, Nicholas Kay, alisema kuwa alishtushwa sana na ukubwa wa mlipuko huo, na kuwataka wale waliotekeleza shambulizi hilo kuchukuliwa hatua za kisheria.

Mji wa Baidoa ulikombolewa na serikali kwa usaidizi wa wanajeshi wa Muungano wa Afrika kutoka kwa wapiganaji wa Al Shabaab miaka miwili iliyopita.

Habari na U Chambuzi

    Author

    CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

    Subscribe to our Mailing List

    We'll never share your Email address.
    +255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com