Tuesday, 13 May 2014

Ehud Olmert jela kwa miaka sita

Posted by mkachu  |  Tagged as:

Ehud Olmert


Mahakama moja nchini Israel imempa kifungo cha miaka sita jela aliyekuwa waziri mkuu nchini Israel Ehud Olmert kwa kosa la kupokea hongo.
Bwana Olmert alipatikana na hatia mwezi machi katika kile kilichojulikana kama 'swala la eneo takatifu' ambapo hongo ilitolewa ili kuharakisha ujenzi wa majumba ya kifahari mjini Jerusalem

Kiongozi huyo alikuwa ameondolewa mashitaka katika kesi tofauti zilizokuwa zikimkabili.
Mashitaka yaliomkabili yalitekelezwa wakati Olmert alipokuwa meya wa mji wa Jerusalem na baadaye akiwa waziri wa serikali.

Ehud Olmert alimrithi Ariel Sharon kama waziri mkuu mnamo mwaka 2006 baada ya Sharon kuugua ugonjwa wa kiharusi.
Alijiuzulu mnamo mwaka 2008.


Habari na U Chambuzi

    Author

    CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

    Subscribe to our Mailing List

    We'll never share your Email address.
    +255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com