Thursday, 8 May 2014

Mamia wauawa na Boko Haram Nigeria

Posted by mkachu  |  Tagged as:


 
Juhudi za serikali dhidi ya kundi hilo hazijaonekana kuzaa matunda

Taarifa kutoka nchini Nigeria, zinasema kuwa mamia ya watu waliuawa katika shambulizi lililofanywa na kundi la wapiganaji wa Boko Haram katika mpaka wa nchi hiyo na Cameroon siku ya Jumanne.

Katika mahojiano na BBC kiongozi mmoja wa eneo hilo, Ahmed Zanna, alisema kuwa washukiwa walivamia mji wa Gamboru Ngala, katika jimbo la Borno, na kuwaua takriban watu 300.

Inaarifiwa wapiganaji hao waliwafyatulia risasi watu kiholela katika soko kuu la eneo hilo.
Mwandishi wa BBC nchini Nigeria anasema ilikuwa vigumu kupata taarifa hizo mapema kwa sababu ya changamoto ya mawasiliano katika jimbo hilo hasa kwa sababu eneo hilo liko mbali sana.
Wakazi wa eneo hilo wanasema kuwa walipata zaidi ya maiti miamoja kutokana na shambulizi hilo.

Habari na U Chambuzi

    Author

    CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

    Subscribe to our Mailing List

    We'll never share your Email address.
    +255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com