Waziri wa mambo ya nje wa Syria, Walid Muallem, ametoa tisho la
kujiondoa kwenye mazungumzo ikiwa hakuna hatua zitakazokuwa zimefikiwa
Jumamosi
Mamilioni ya watu wameachwa bila makao kutokana na vita nchini Syria
Waakilishi wa serikali ya Syria katika mazungumzo ya amani kati ya
wanaharakati na serikali, wametishia kuondoka kwenye mazungumzo hayo ya
amani ikiwa mazungumzo muhimu hayatakuwa yameanza ifikapo Jumamosi.
Waziri wa mambo ya nje wa Syria, Walid Muallem, ametoa tisho la
kujiondoa kwenye mazungumzo baada ya kukutana na mjumbe maalum wa UN
nchini Syria Lakhdar Brahimi.
Bwana Brahimi anatarajiwa kukutana na upande wa upinzani baadaye Ijumaa.
Duru zinasema kuwa mazungumzo yamekumbwa na changamoto hasa kwa kuwa pande zote mbili zina misimamo mikali.
Mgogoro wa kisiasa nchini Syria, umesababisha vifo vya watu 100,000 kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.
Ghasia hizo pia zimesababisha watu milioni 9.5
kutoroka makwao, na kusababisha hali mbaya ya kibinadamu ndani ya Syria
na katika nchi jirani.
Hii ni siku ya tatu ya mazungumzo mjini Geneva lakini mkutano wa kwanza rasmi ambapo mazungumzo yanaanza.
Kulikuwa na matumaini ya mkutano wa ana kwa ana
kati ya serikali na wanaharakati, lakini baadaye bwana Brahimi alifanya
mazungumzo na kila upande.
Pande hizo zinalaumiana kwa changamoto hiyo.
Friday, 24 January 2014
Browse: Home
» Syria yatishia kujiondoa Geneva
Syria yatishia kujiondoa Geneva
Posted by mkachu | Tagged as:
Habari na U Chambuzi
HALI YA HEWA
TANGAZANASI
MTANDAO WA KIJAMII
ZILIZO SOMWA ZAIDI
-
eshi la Marekani limefanya shambulizi la makombora dhidi ya mtu anayeshukiwa kuwa mmoja wa viongozi wa al-Shabaab nchini Somalia. ...
-
Chama Cha Mapinduzi (CCM) party stalwart Rostam Aziz has earned USD 240 million (about Tsh. 384,000,000,000/-) from selling part of his st...
-
Wanaume wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mw...
-
Kundi moja la wanawake walio na hisia za kimapenzi na mapadre wa kikatoliki wamemuandikia barua kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa F...
-
Madrasa hii ilianzishwa mnamo mwaka 2005 ikiwakama madrasa ya nyumbani ikiwa ndani ya jiji la Mwanza katika kito ngoji cha Bugando je...
-
Juhudi za serikali dhidi ya kundi hilo hazijaonekana kuzaa matunda Taarifa kutoka nchini Nigeria, zinasema kuwa mamia ya watu waliuawa...
-
Baadhi ya wanawake wengi wa hapa mjini wameanza kutumia style mpya ya kugundisha nywele aka wiving katika vichwa vyao kwa kutumia gu...
-
Marekani kusaidia kuwasaka wasichana waliotekwa na Boko Haram Serikali ya Nigeria inasema kuwa iko tayari kuzingatia mbinu zote zitakazo...
-
Baadhi hutengeza maji ya sharubati kwa kuichanganya na matunda Baadhi wanaamini kuwa Kondo la nyuma huwa na madini mengi ambayo hayapaswi...
-
Inspector Henry akiwasihi mahabusu hao wawili wanaotuhumiwa kwa kesi za mauaji, kuachia mlingoti wa Bendera ya Taifa na kurudi kwenye chum...
MITANDAO YA KIJAMII
TAFUTA HABARI ZILIZO SOMWA NYUMA
Pages
WALIO TEMBELEA
Powered by Blogger.
TANGAZA NASI
kwama Matangazo wasiliana nasi kupitia anuani zifuataz
Email:
mohamedwaziri295@gmail.com
mohamedwaziri21@yahoo.com
contact us:
0762118805
0658118804
info@islamicnews.blogspot.com
Wote mnakalibishwa
Email:
mohamedwaziri295@gmail.com
mohamedwaziri21@yahoo.com
contact us:
0762118805
0658118804
info@islamicnews.blogspot.com
Wote mnakalibishwa
Total Pageviews
3208
Labels
DOWNLOAD QASWIDA
islamic
islami news
Social Icons
islamic
Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...