
Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan
Rais wa Nigeria Goodluck Jonathana ameagiza shule zote na ofisi za
serikali katika mji mkuu wa Abuja nchini humo zifungwe wakati wa siku
tatu za Mkutano wa Uchumi wa Dunia World Economic Forum utakaanza nchini
humo jumatano ijayo.
Serikali imesema hatua hiyo ni kuarahisisha misafara ya magari. Lakini
suala la kuimarisha ulinzi huenda ni mambo yaliyosababisha hatua hiyo
Mwandishi wa BBC Will Ross anasema akiwa Abuja.
Ulinzi mkali umehaidiwa kwa wageni wapatao 1000 wakati wa mkutano huo.
Rais Jonathan amesema polisi wapatao 5000 na
wanajeshi watafanya doria na kushika hatamu za ulinzi wakati wa mkutano
huo utakaoanza wiki ijayo
Waziri Mkuu wa China Li Keqiang na Marais wa Rwanda, Senegal na Kenya ni miongoni mwa viongozi wa juu wa nchi watakaohudhuria.
Mji wa Abuja katika siku arobaini zilizopita ulishambuliwa kwa matukio mawili ya mabomu yaliyoua watu wapatao tisini.
Rais Jonathan amesema polisi wapatao 5000 na wanajeshi watafanya doria
na kushika hatamu za ulinzi wakati wa mkutano huo utakaoanza wiki ijayo.
Baadhi ya wanawake wakiandama kutaka serikali kuchukua hatua zaidi kuwaokoa wasichana waliotekwa
Kundi la Boko Haram linadaiwa kuhusika na mashambulizi hayo.
Kundi hilo hilo pia linatuhumiwa kuwateka nyara
wasichana zaidi ya 200 katika shule moja kwenye mji wa Borno uliopo
Kaskazini Mashariki mwa Nigeria siku arobaini zilizopita.
Jina la kundi hilo lenye tafsiri ya "Kupiga
marufuku elimu ya nchi za Maghiribi" kwa lugha ya Kihausa kimekuwa
kikiendesha mashambulizi kadhaa kaskazini mwa Nigeria katika siku za
hivi karibuni.
Baadhi ya wanawake wakiandama kutaka serikali kuchukua hatua zaidi kuwaokoa wasichana waliotekwa
Kundi la Boko Haram linadaiwa kuhusika na mashambulizi hayo.
Kundi hilo hilo pia linatuhumiwa kuwateka nyara
wasichana zaidi ya 200 katika shule moja kwenye mji wa Borno uliopo
Kaskazini Mashariki mwa Nigeria siku arobaini zilizopita.
Jina la kundi hilo lenye tafsiri ya "Kupiga
marufuku elimu ya nchi za Maghiribi" kwa lugha ya Kihausa kimekuwa
kikiendesha mashambulizi kadhaa kaskazini mwa Nigeria katika siku za
hivi karibuni.
Wanawake walivaa nguo nyekundu kuonyesha kuguswa na wasichana waliotekwa
Inakadiriwa watu wapatao 1500 wameuawa katika
mashambulizi yaliyofanywa na kundi hilo pamoja na operesheni ya majeshi
ya serikali wakati wa kulisaka kundi hilo.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani John Kerry
ambaye anafanya ziara barani Afrika amesema Marekani itafanya kila
liwezekanalo kuisaidia serikali ya Nigeria kuwaokoa na kurudisha
nyumbani wasichana mia mbili waliotekwa na kundi la waislamu
linalosadikiwa kuwa la Boko Haram siku kumi tisa zilizopita
Read more »