Tuesday 20 May 2014

Pistorius kufanyiwa uchunguzi wa akili

Posted by mkachu  |  Tagged as:



     
Pistorius akiwa mahakamani

Jaji katika kesi inayomkabili Oscar Pistorius anasema kuwa mwanariadha huyo lazima aanza kufanyiwa uchunguzi wa kiakili kuanzia Jumatatu wiki ijayo kwa mwezi mmoja kubaini hali ya akili yake alipomuua mpenzi wake Reeva Steenkamp.
Jaji Thokozile Masipa aliamuamuru Pistorius kua awe anakwenda katika hospitali ya maradhi ya kiakili ya Weskoppies mjini Pretoria kila siku kuanzia tarehe 26 mwezi Mei.
Amri ya jaji inakuja baada ya shahidi mmoja wa upande wa mashitaka kusema kuwa mwanariadha huyo anakumbwa na matatizo ya kuzongwa na mawazo pamoja na kuwa na wasiwasi wakati wote
Bwana Pistorius amekanusha madai ya kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp kusudi
Anasema kwamba kwa bahati mbaya alimpiga risasi kupitia mlango wa choo baada ya kushikwa na wasiwasi akidhani kuwa alikuwa jambazo aliyevamia nyumba yake.


Habari na U Chambuzi

Author

CONTACT ME FOR WEB AND BLOG DESIGNING...

Subscribe to our Mailing List

We'll never share your Email address.
+255 (762) 118-805 mohamedwaziri295@gmail.com